Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 15, 2012

Afrika, ajenda kuu ya kikao cha Francophone Kinshasa



Afrika, ajenda kuu ya kikao cha Francophone KinshasaUungaji mkono kwa bara la Afrika na juhudi za kutatuliwa migogoro katika nchi zilizokumbwa na migogoro barani humo, ndiyo ajenda kuu ya kikao cha kwanza cha wakuu wa nchi zinazozungumza lugha ya Kifaransa Francophone kinachoendelea huko Kinshasa mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Taarifa zinasema kuwa, wakuu wa Francophone wamejikita zaidi katika kujadili  migogoro na machafuko ya kisiasa yaliyoko barani Afrika. Taarifa kutoka Kinshasa zinasema kuwa, wakuu hao wameafikiana pia juu ya kutolewa maazimio yenye lengo la kukomesha mgogoro wa mashariki mwa Kongo, na migogoro  mingine ya Mali, Madagascar na Guinea Bissau. Nchi za Senegal na Vietnam zimetangaza kuwania nafasi ya kuandaa mkutano ujao wa Francophone hapo mwaka 2014.

No comments:

Post a Comment