Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, October 30, 2012

Wanamgambo wa ash Shabab wawaonya Waingereza



Wanamgambo wa ash Shabab wawaonya WaingerezaKundi la wanamgambo wa ash Shabab nchini Somalia limetishia kufanya mashambulizi dhidi ya Uingereza.
Shirika la Habari la Ufaransa limenukuu taarifa ya kundi hilo ikisema kuwa: Uingereza lazima ilipe gharama kubwa za vita vyake dhidi ya Uislamu na kitendo chake cha kumrejesha Sheikh Abu Hamza wa Uingereza nchini Marekani.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ash Shabab imetishia kufanya mashambulizi makali zaidi dhidi ya London kuliko yale ya tarehe 7 na 21 Julai 2005.
Itakumbukwa kuwa, miripuko ya mabomu ya tarehe 7 Julai 2005 ilipelekea watu 52 kuuwa mjini London Uingereza. Wiki mbili baadaye miripuko mingine minne ya mabomu ilitokea kwenye mfumo wa usafiri wa umma mjini humo.
Somalia haina serikali kuu tangu mwaka 1991 na tangu wakati huo hadi hivi sasa makundi mbalimbali ya watu wenye silaha yamekuwa yakijitokeza nchini humo kwa ajili ya kujidhaminia mambo tofauti.

No comments:

Post a Comment