Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, February 1, 2013

Jinai za kivita za Israel dhidi ya Wapalestina


Kijana Mpalestina akivunjiwa haki na wanajeshi wa IsraelWachunguzi wa haki za binaadamu katika Umoja wa Mataifa wameutaka utawala wa Israel kusitisha upanuzi wa vitongoji vya waloezi wa Kizayuni na kuwaondoa walowezi nusu milioni katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan. Katika taarifa iliyotolewa Alkhamisi jopo la Umoja wa Mataifa limesema hatua ya kujenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Palestina ni jambo ambalo linaweza kuhesabiwa kuwa jinai za kivita. Ripoti hiyo imeongeza kuwa ulowezi wa Wazayuni umechangia ukiukaji wa haki za Wapalestina kwa njia nyingi.

Bi. Christine Chanet aliyeoongoza jopo hilo amesema Israel inakiuka Mkataba wa Geneva kwa kujenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Palestina. Baada ya kutolewa ripoti hiyo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa Israel inapaswa kusitisha harakati za ujenzi wa vitongoji katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu ikiwa ni pamoja na Quds Mashariki. Mamlaka ya Ndani ya Palestina imetishia kuichukulia Israel hatua za kisheria katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) iwapo Tel Aviv itaendeleza ujenzi katika maeneo ya Palestina inayoyakaliwa kwa mabavu.

No comments:

Post a Comment