Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, February 2, 2013

Wafungwa Waislamu UK walazimishwa kula nguruwe


Wafungwa Waislamu UK walazimishwa kula nguruwe
Haki za Waislamu nchini Uingereza zimeendelea kukiukwa huku wafungwa wa Kiislamu wanaotumikia vifungo katika magereza ya nchi hiyo wakilazimishwa kula nyama ya nguruwe. Shirika moja la kutetea haki za binadamu limetangaza kuwa, serikali ya Uingereza imekuwa ikikiuka haki za wafungwa wa Kiislamu katika magereza ya nchi hiyo. Taarifa zaidi zinasema, serikali ya Uingereza imekataa kupeleka nyama halali kwa ajili ya wafungwa wa Kiislamu katika magereza ya nchi hiyo na badala yake imekuwa ikiwalazimisha wafungwa hao wa Kiislamu kula nyama ya nguruwe ambayo kwa mujibu wa mafundisho ya dini yao ni haramu.
Imeelezwa kuwa, katika baadhi ya magereza wahusika katika magereza hayo wamekuwa wakipeleka nyama ya nguruwe na kupuuza kwamba, kuna wafungwa ambao ni wafuasi wa dini ya Kiislamu. Taarifa zaidi zinaeleza kuwa, katika baadhi ya magereza nyama ya matumizi kwa ajili ya wafungwa imepatikana ikiwa imechanganywa na nyama ya nguruwe. Shirika linalotetea mageuzi katika magereza nchini Uingereza limetoa wito wa kufanyika uchunguzi kuhusiana na ukiukaji wa haki za binadamu katika magereza ya nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment