Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, February 1, 2013

Wasiwasi wa UN kuhusu harakati za al Shabab Somalia

    Waasi wa al Shabab, Somalia
Umoja wa Mataifa umeonya kuwa wapiganaji wa kundi la al Shabab wanagali wanaendeleza harakati zao Somalia jambo ambalo linaweza kuwa kizingiti katika marekebisho ya kisiasa na kiusalama nchini humo.
Katika taarifa Umoja wa Mataifa umesema baada ya kumalizika malumbano ya kisiasa Somalia mwaka 2012 tishio kubwa zaidi sasa ni kundi la kigaidi la al Shabab.
Wakati huo huo Mkuu wa Masuala ya Kisiasa katika Umoja wa Mataifa Jeffery Feltman amesema umoja huo umejizatiti kusaidia Somalia kujenga amani ya kudumu. Ameyasema hayo Alkhamisi mjini Mogadishu baada ya mazungumzo yake na vinogozi wa Somalia.

No comments:

Post a Comment