Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, February 2, 2013

Watu 35 wauawa katika mapigano nchini Pakistan


Watu 35 wauawa katika mapigano nchini PakistanWatu wasiopungua 35 wameuawa katika shambulio lililofanywa mapema leo na kundi la wanamgambo kwenye kituo kimoja cha upekuzi cha jeshi huko Lakki Marwat kaskazini magharibi mwa Pakistan. Kundi la Taliban ya Pakistan limetangaza kuhusika na shambulio hilo lililoandamana na ufyatulianaji risasi na uvurumishaji makombora kwenye nyumba moja. Kundi hilo limedai kuwa shambulio hilo ni jibu kwa shambulio la mwezi uliopita lililofanywa na ndege isiyo na rubani ya Marekani huko Waziristan Kaskazini na kupelekea kuuawa makamanda wawili wa kundi hilo. Msemaji wa Taliban amesema serikali ya Pakistan imekuwa ikishirikiana na Marekani katika mashambulio yake ya ndege zisizo na rubani ndani ya ardhi ya Pakistan na kwamba shambulio hilo ni la kulipiza kisasi kwa mauaji ya Faisal Khan na Toofani,
makamanda hao wawili  wa kundi hilo. Afisa usalama wa Pakistan amesema wanamgambo 12 na askari 13 waliuawa katika mapigano hayo yaliyoendelea kwa muda wa masaa manne huku viwiliwili viwili vya waliouawa vikiwa na mikanda ya mabomu ya kujitolea mhanga. Afisa huyo wa serikali ya Islamabad ameongeza kuwa wanamgambo wa Taliban pia waliilenga kwa makombora nyumba moja na kuua watu 10 wa familia moja wakiwemo watoto watatu.

No comments:

Post a Comment