Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, February 25, 2013

Kuna njama za kupandikiza chuki za kidini Zanzibar


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amesema kuwa, kuna njama za kupandikiza chuki za kidini visiwani Zanzibar huko Tanzania. Maalim Seif ametahadharisha kuwa huenda kuna watu wenye nia mbaya ambao wameamua kuyatumia matukio ya kuuawa na kujeruhiwa viongozi wa kidini, kujenga chuki baada ya kuona Wazanzibari hivi sasa ni wamoja. Maalim Seif amesema hayo alipokuwa akihutubia katika hafla ya Maulid ya Kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W), huko Wilaya ya Wete, Kaskazini Pemba. Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF amesema,
 inasikitisha kuona kuwa, wapo viongozi wenye nia chafu dhidi ya Zanzibar na wenye tabia ya kutoa kauli za kujenga chuki na fitna miongoni mwa Wazanzibari chini ya kivuli cha matukio hayo. Amesema, kinachoonekana kuna ajenda imetayarishwa ya kutaka kulazimisha chuki za kidini Zanzibar, licha ya kuwa kisiwa hicho kina historia ya dahari ya watu kuvumiliana na kuishi kwa pamoja. Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amewataka wananchi wote wa Zanzibar hivi sasa wawe macho na ajenda zinazolengwa kuwavuruga, na waendelee kuishi kwa mshikamano na umoja kama ambavyo wamekuwa wakiishi.

Na Salum Bendera

No comments:

Post a Comment