Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, February 2, 2013

WAZAYUNI WANADHIBITI VYOMBO VYA HABARI DUNIANI



Dakta Muhammad Sarafraz Mkuu wa Kitengo cha Matangazo ya Ng'ambo wa Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran IRIB amesema kuwa, mfumo wa Kizayuni unadhibiti kanali zote za habari ulimwenguni. Akizungumzia vita vipya dhidi ya vyombo vya kupasha habari vya Iran, Dakta Sarafraz amesema kuwa, iwapo itaanzishwa kanali ya habari itakayokuwa tofauti na kanali  nyinginezo, bila shaka  mfumo wa Kizayuni utaingilia kati na kuifuta kanali hiyo. Ameongeza kuwa, tarehe 28 Januari 2013 serikali ya Uhispania ilichukua maamuzi yanayokinzana wazi na uhuru wa kujieleza pale ilipotoa amri ya kukatwa matangazo ya kanali ya HispanTV ya Iran inayotangaza matangazo yake kwa lugha ya Kihispania. Dakta Sarafraz ameongeza kuwa, sehemu ya hisa ya shirika la huduma za satalaiti la Hispasat inafungamana na shirika la Eutelsat; na Mkurugenzi wa Eutelsat ni Mfaransa mweye asili ya Kizayuni ambaye hivi karibuni amekuwa akivisakama vyombo vya kupasha habari vya Iran huko Ulaya. Mkurugenzi wa Kitengo cha Matangazo ya Ng'ambo wa IRIB ameongeza kuwa, Marekani inajidai kuwa ni mtetezi mkubwa wa haki za binadamu, uhuru wa kujieleza na demokrasia, amma inawaunga mkono madikteta wa Bahrain na Saudia Arabia katika kuwakandamiza wananchi wa nchi hizo.

No comments:

Post a Comment