Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, March 29, 2013

Picha za Muonekano wa Ghorofa lililoanguka Asubuhi ya Leo Kariakoo












Mabaki ya jengo hilo lililoporomoka jijini da es salaam amablo lipo barabara ya morogoro mtaa wa indiana.Huku ni mashuhuda watukio hilo wakiwa eneo hilo muda huu..Maiti zaidi zinaokolewa bado idadi kamili haijafahamika mpaka sasa.Endelea kupitia audifacejackson blogspot kwa taarifa ziadi

Monday, March 25, 2013

Uamsho haina account wala page facebook



Masoud Khamis Al-Bimani

Jumuia ya UAMSHO na Mihadhara ya Kiislam Zanzibar haina account wala page ya Facebook, lakini kuna watu kwa makusudi wameamua kutengeneza Page ya Uamsho hapa FB, kwa lengo la kuitia Doa jumuiya, anakua anapost vitu visivyo na Maana, kwa lengo la kuupotosha Umma tujihadhari na watu hawa.

Kesi ya Uamsho yasomwa upya, yapangiwa Jaji Fatma



KESI ya jinai inayowakabili viongozi wa Dini wa Jumuiya ya Uwamsho na
Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) imeanza kusomwa upya leo katika Mahakama Kuu ya Zanzibar baada ya maamuzi ya awali kutenguliwa.

Kesi hiyo namba 9 ya mwaka 2012 ilisomwa mbele ya Jaji Fatma Hamid
Mahmoud na Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Ramadhan Nassib, ambae
aliwataja washitakiwa hao kuwa ni Farid Hadi Ahmed (41) mkaazi wa Mbuyuni,

Wednesday, March 20, 2013

Rwanda yawanyima viza wataalamu wa UN


Rwanda yawanyima viza wataalamu wa UN
Rwanda imekataa kutoa viza kwa maafisa wawili wa timu ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa iliyoituhumu Kigali mwaka jana kuwa inawapa silaha waasi wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kuwataja kuwa watu wenye upendeleo.

Al Qaeda wamuua mateka wa Kifaransa


Al Qaeda wamuua mateka wa Kifaransa
Mtandao wa al Qaeda wa kaskazini mwa Afrika umetangaza kuwa umemuua mateka wa Kifaransa katika kulipiza kisasi uingiliaji wa kijeshi wa Ufaransa nchini Mali. Mateka huyo wa Kifaransa kwa jina la Phillippe Verdon alikatwa kichwa na mtandao huo wa al Qaida tarehe kumi mwezi huu katika kile kundi hilo lilichokisema kuwa ni kulipiza kisasi cha mashambulizi yaliyoanzishwa na Paris huko Mali. Verdon alikuwa mmoja kati ya raia wawili wa Ufaransa waliotekwa nyara mwezi Novemba mwaka juzi huko kaskazini mwa Mali katika mji wa Hombori. 

Polisi ya Misri yamtia mbaroni binamu wa Gaddafi


Polisi ya Misri yamtia mbaroni binamu wa Gaddafi
Polisi ya Misri imesema kuwa imemtia mbaroni binamu na aliyekuwa mpambe wa karibu wa Muammar Gaddafi kiongozi wa zamani wa Libya. Hapo jana maafisa wa Misri walisema kuwa Ahmed Gaddaf al Dam alitiwa nguvuni baada ya vikosi vya usalama kuizingira nyumba yake katika kitongoji cha Zamalek huko Cairo. Afisa mmoja wa Misri amesema kuwa afisa huyo wa zamani wa intelijinsia wa utawala wa Gaddafi atakabidhiwa kwa maafisa wa Libya hivi karibuni. Baada ya kuzingirwa nyumba yake kwa masaa kadhaa huko katikati mwa Cairo, binamu huyo wa Muammar Gaddafi alisikika akizungumza na kanali moja ya televisheni kwa njia ya simu na hapa ninamnukuu" tulifika hapa kwa mwaliko wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri na baraza la kijeshi, sisi si magaidi wa kuweza kushambuliwa namna hii," mwisho wa kumnukuu.  

Tuesday, March 19, 2013

37 wafariki dunia katika ajali ya basi India


37 wafariki dunia katika ajali ya basi IndiaPolisi ya India imetangaza kuwa kwa akali watu 37 wamepoteza maisha na wengine 17  kujeruhiwa, baada ya basi la abiria walilopanda kupoteza mwelekeo na kutumbukia katika  mto wa Jagbudi magharibi mwa nchi hiyo.
Polisi ya India imeeleza kuwa, ajali hiyo mbaya imetokea mapema leo alfajiri katika wilaya ya Maharashtra. Polisi ya Usalama barabarani nchini India imeeleza kuwa, basi hilo lilikuwa likitokea katika mji wa Goa na kuelekea Mumbai; na kwamba  dereva wa basi hilo alishindwa kulidhibiti na kutumbukia mtoni. Polisi imeeleza kuwa, ajali hiyo imetokea umbali wa kilomita 350 kusini mwa Mumbai.
Polisi imeeleza kuwa, watu wasiopungua 17 wamejeruhiwa akiwemo dereva wa basi hilo, ambaye hali yake imeelezwa kuwa ni mahututi. Taarifa za awali zinasema kuwa, ndani ya basi hilo kulikuwa na idadi kadhaa ya watalii kutoka nje ya nchi hiyo.

Siasa za Wamagharibi ni za kindumakuwili


Siasa za  Wamagharibi ni za kindumakuwili
Katibu Mkuu wa Harakati ya Ukombozi ya Bahrain amezikosoa vikali siasa za kindumakuwili za Magharibi kuhusiana na matukio ya kieneo na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Bahrain unaofanywa na utawala wa Aal Khalifa wa nchi hiyo.
Saeed al Shahabi ameongozana na maelfu ya wapinzani wa Bahrain na kukusanyika mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu wa Uingereza mjini London na kusema kuwa, uungaji mkono wa kibubusa wa Marekani na Uingereza kwa utawala wa Aal Khalifa umesababisha utawala huo kuvimba kichwa na kupuuza misingi ya haki za binadamu.
Ameongeza kuwa, siasa za kindumakuwili za nchi za Magharibi sio za kikhlaki na amebainisha kuwa, Washington na London zinapaswa kukomesha uungaji mkono wao kwa utawala wa Bahrain ambao unatenda jinai za mauaji, kuwafunga na kuwashikilia korokoroni wanaharakati na kuwatesa wananchi wa nchi hiyo wanaume na wanawake.

Boko Haram waua walimu watatu Nigeria


Wanamgambo wa Boko Haram wakiwa wamejizatiti kwa silaha NigeriaWalimu watatu wameuawa katika mashambulio yaliyofanywa na watu wenye silaha dhidi ya shule mbili huko kaskazini mashariki mwa Nigeria. Walimu hao waliuawa jana katika mashambulio mawili yaliyotekelezwa na watu wenye silaha wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa kundi la Boko Haram katika mji wa Maiduguri unaopatikana katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Aidha wanafunzi kadhaa walijeruhiwa katika mashambulizi hayo. Kabla ya hapo pia, watu 25 waliuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa baada ya kutokea milipuko mitano katika mji wa Kano kaskazini mwa Nigeria. Hadi sasa hakuna mtu au kundi lolote lililotangaza kuhusika na mashambulio hayo, lakini kundi la Boko Haram linashukiwa kuwa ndilo lililotekeleza mashambulio hayo kwa vile limekuwa likitekeleza mashambulio kama hayo katika maeneo tofauti ya nchi hiyo ya Magharibi mwa Afrika.

Wazimbabwe waipigia kura ya ndio katiba mpya


Wazimbabwe waipigia kura ya ndio katiba mpya
Matokeo yasiyo rasmi ya kura ya maoni ya katiba mpya nchini Zimbabwe, yanaonyesha kwamba, wananchi wameipigia kura ya ndio katiba hiyo ambayo inapunguza madaraka ya rais wa baadaye wa nchi hiyo. Ripoti zilizosambazwa leo kutoka vituo vya kuhesabu kura, zinaonyesha kuwa, watu milioni tatu na laki moja kati ya watu milioni tatu na laki nne waliofika kwenye vituo vya kupigia kura nchini humo, wameipigia kura ya ndio katiba mpya ya nchi hiyo ya kusini mwa Afrika inayokabiliwa na mgogoro mkubwa wa kiuchumi. Gazeti la Herald limeripoti kuwa, watu laki mbili wameipigia kura ya hapana katiba hiyo. Kwa mujibu wa takwimu rasmi za nchi hiyo, Wazimbabwe milioni sita pekee ndio waliokamilisha masharti ya kupiga kura nchini. Ilitarajiwa kuwa, hadi kufikia jioni ya leo, Tume ya Uchaguzi nchini humo ingekuwa imekamilisha kazi za kuhesabu kura na kutangaza matokeo rasmi ya kura hiyo.

Mapigano kati ya jeshi na waasi Sudan Kusini


Waasi wenye silaha nchini Sudan KusiniShirika la Msalaba Mwekundu limetangaza kuwa, zaidi ya watu 60 wamejeruhiwa katika mapigano ya hivi karibuni kati ya jeshi la Sudan Kusini na kundi moja la waasi nchini humo. Shirika hilo limeongeza kuwa, katika kipindi cha wiki mbili zilizopita karibu watu 62 waliojeruhiwa katika apigano hayo walitibiwa katika kituo kimoja cha afya cha shirika hilo na kwamba. Mmoja wa viongozi wandamizi wa shirika hilo amenukuliwa akisema kuwa, idadi rasmi ya maafa yaliyotokana na machafuko hayo ya pande mbili haijafahamika kutokana na kwamba, hadi sasa hakuna taasisi yoyote iliyofika eneo la tukio na kufanya uchunguzi. Ameongeza kuwa, kutokana na viongozi wa Juba kukosa ripoti kamili ya mapigano hayo, idadi ya wahanga inaweza kupindukia ile iliyotajwa hapo awali. Hivi karibuni mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, alielezea kusikitishwa kwake na vitendo vya kikatili vinavyofanywa na Jeshi la Sudan Kusini dhidi ya waasi wanaoongozwa na David Yauyauambao wanaipinga serikali ya Juba.

Monday, March 18, 2013

Watu 10 wauawa kwenye mlipuko nchini Somalia


Watu 10 wauawa kwenye mlipuko nchini Somalia
Habari kutoka Mogadishu, mji mkuu wa Somalia zinasema kuwa, kwa akali watu 10 wamefariki dunia na makumi ya wengine kujeruhiwa kufuatia mlipuko mkubwa wa bomu uliotokea karibu na ukumbi wa kitaifa wa michezo ya kuigiza.
Habari zaidi zinasema kuwa, bomu hilo lilikuwa limetegwa kwenye gari na kwamba Mkuu wa Usalama wa Mogadishu ndiye alikuwa mlengwa mkuu. Haijabainika wazi iwapo mkuu huyo ameuawa au la.
Kundi la wanamgambo la Al-shabab tayari limedai kuhusika na shambulio hilo. Kundi hilo limeapa kumuondoa madarakani Rais Hassan Sheikh Mohamud, aliyechaguliwa na bunge la Somalia mwaka uliopita. Hii ni katika hali ambayo, wanamgambo hao wanaripotiwa kuuteka mji wa Hudur wa kusini mwa Somalia.