Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, June 10, 2013

Askari wa Misri kutoshiriki uchaguzi hadi 2020


Askari wa Misri kutoshiriki uchaguzi hadi 2020
Askari polisi na wanajeshi wa Misri hawatashiriki kwenye uchaguzi wowote hadi mwaka 2020. Bunge la Misri limesitisha hadi mwaka 2020 mpango wa kuwapa wanajeshi na askari polisi wa nchi hiyo haki ya kupiga kura. Awali Naibu Waziri wa Ulinzi anayehusika na masuala ya sheria na katiba wa Misri alitoa pendekezo kwa kamati ya bunge la nchi  hiyo kuandaa mpango wa kuwapatia wanajeshi na askari polisi haki ya kupiga kura kwenye chaguzi mbalimbali zitakazofanyika nchini humo. Mahakama ya Katiba ya Misri mwezi Mei mwaka huu ilitangaza kuwa, kwa mujibu wa katiba mpya ya nchi hiyo, askari polisi na wanajeshi wana haki ya kushiriki kwenye chaguzi nchini humo.

No comments:

Post a Comment