Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, June 18, 2013

Rais wa Gambia: Magharibi wanaua watu ovyo


Rais wa Gambia: Magharibi wanaua watu ovyo
Rais Yahya Jammeh wa Gambia amezikosoa vikali nchi za Magharibi kwa kufanya mauaji ya raia wasio na hatia katika nchi mbalimbali za dunia kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi. Rais Jammeh aliyasema hayo wakati akiwahutubia wakazi wa eneo la pwani la magharibi ya nchi hiyo na kuongeza kuwa, vita vya nchi za Magharibi dhidi ya ugaidi ni vita dhidi ya raia wasio na hatia. Akiashiria mauaji ya ndege za Marekani zisizo na rubani na mauaji yanayofanywa dhidi ya watu wanaodhaniwa tu kuwa ni magaidi, Rais Jammeh amesema, kwa hakika Magharibi wanafanya mauaji ya raia wasio na hatia duniani. Aidha amesisitiza kuwa, watu wengi wanaouliwa na ndege hizo za kigaidi zisizo na rubani si magaidi na kwamba, madai ya madola hayo ya kibeberu ya kupambana na ugadi hayana ukweli wowote na yamejaa upotoshaji.

No comments:

Post a Comment