Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, June 1, 2013

Serikali ya Ghana yaondoa ruzuku ya fueli


Serikali ya Ghana yaondoa ruzuku ya fueliSerikali ya Ghana imeondoa ruzuku ya bidhaa za fueli yakiwemo mafuta ya petroli, mafuta ya dizeli na gesi ili kusaidia kupunguza nakisi katika bajeti yake. Uamuzi huo umetangazwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Taifa ya Bidhaa za Petroli (NPA) Alex Mould ambaye amesisitiza kuwa utekelezaji wa uamuzi huo umeanza rasmi leo. Kutokana na kuchukuliwa hatua hiyo bei ya mafuta ya petroli itapanda kwa asilimia 3 na bei ya mafuta ya dizeli kwa asilimia 2. Ghana imekuwa moja ya nchi zenye uchumi unaokuwa kwa kasi duniani tangu ilipoanza kuzalisha mafuta mwaka 2010, lakini serikali imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya kudhibiti nakisi ya bajeti ya matumizi yake na uthabiti wa sarafu ya nchi hiyo ya cedi. Nakisi ya bajeti ilifikia kiwango asilimia 12.1katika mwaka uliopita wa 2012 mara mbili zaidi ya lengo lililowekwa la asilimia 6.7. Uamuzi wa kuondoa ruzuku katika bidhaa za fueli ulikuwa utekelezwe tangu mwaka uliopita nchini Ghana lakini ulicheleweshwa kwa sababu ya uchaguzi wa rais uliofanyika mwezi Disemba kufuatia kifo cha aliyekuwa rais wa nchi hiyo John Atta Mills…/

No comments:

Post a Comment