Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, June 16, 2013

Askari watatu wauawa katika mapigano Libya


Askari watatu wauawa katika mapigano Libya
Mapigano kati ya watu wenye silaha na jeshi pamoja na polisi ya Libya yamesababisha kwa uchache askari watatu kuuawa na wengine kujeruhiwa. Mapigano hayo yametokea baada ya watu wenye silaha mjini Bengazi mashariki mwa Libya, kufanya maandamano. Hayo yamethibitishwa na kikosi maalumu cha jeshi la nchi hiyo kinachofahamika kwa jina la ‘Swaiqah’ na kuongeza kuwa, mapigano hayo yamejiri mapema leo asubuhi ambapo katika mapigano hayo, kulitumiwa pia maguruneti na aina nyingine ya silaha nzito. Aidha habari zaidi zinasema kuwa, mapigano yalijiri baada ya waandamanaji waliokuwa na silaha kufanya shambulizi dhidi ya ngome ya kilojestiki ya kikosi hicho cha Saiqah na kwamba, hadi sasa bado milio ya risasi na milipuko inaendelea kusikika karibu na kambi ya kikosi hicho cha Saiqah na askari wa miamvuli hapo mjini Bengazi.

No comments:

Post a Comment