Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, June 10, 2013

Russia wataka zitumike Hijab mashuleni


Russia wataka zitumike Hijab mashuleniMkuu wa Muungano wa Wanawake wa Kiislamu nchini Russia amesisitiza juu ya kutumiwa vazi la Kiislamu Hijab ya Kiislamu katika maeneo ya umma bila ya kukinzana sheria hiyo ya Kiislamu na ile ya serikali ya Russia. Nailya Ziganshina amesema kuwa, utumiwaji wa vazi la Hijab kwa wanawake wa Kiislamu hakukinzani na sheria za sekta ya elimu nchini humo, yakiwemo mashule. Bi Nailya Ziganshina amesema kuwa, uvaaji huo wa Hijab unakwenda sambamba na mila, desturi na utamaduni wa kidini katika jamii ya nchi hiyo na kusisitiza kuwa, utumiaji wa Hijab haukinzani na mafunzo kwa watoto kwenye shule za nchi hiyo. Inafaa kuashiria hapa kuwa, ni miaka mingi sasa kwa serikali ya Russia kupiga marufuku uvaaji wa Hijab kwenye mikusanyiko ya umma na hasa mashuleni , suala ambalo limesababisha matatizo makubwa kwa wafuasi wa dini ya Kiislamu nchini Russia.

No comments:

Post a Comment