Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, June 10, 2013

Matokeo ya uchaguzi Madagascar kutotambuliwa


Matokeo ya uchaguzi  Madagascar kutotambuliwa
Serikali ya Ufaransa imetangaza kwamba, haitotambua matokeo ya uchaguzi wa rais nchini Madagascar iwapo wagombea fulani watashiriki Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Ufaransa, Philippe Lalliot amewataja rais wa sasa Andry Rajoelina, Lalao Ravalomanana; mke wa rais wa zamani aliyepinduliwa na rais wa zamani Didie Ratsiraka na kusema kwamba, kushiriki kwao kwenye uchaguzi ujao kutaendelea kuitumbukiza Madagascar kwenye mgogoro wa kisiasa ulioanza mwaka 2009 kufuatia mapinduzi yaliyomuondoa madarakani, Mark Ravalomanana. Msimamo wa Ufaransa unakwenda sanjari na ule wa Umoja wa Afrika AU na Jumuiya ya SADC ambazo zimetaka wanasiasa hao kuheshimu makubaliano ya Maputo yanayowazuia kuwania urais. Hii ni katika hali ambayo Mahakama ya kilele ya Madagascar imeamua kwamba watatu hao wanaweza kuwania urais kwani hakuna sheria ya nchi yao inayowazuia kufanya hivyo. Uchaguzi wa rais unatarajiwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu.

No comments:

Post a Comment