Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, June 16, 2013

Misri yakata uhusiano wa kidiplomasia na Syria


 Misri yakata uhusiano wa kidiplomasia na Syria
Rais Mohammad Mursi wa Misri ametangaza kuwa nchi yake imekata kabisa uhusiano wa kidiplomasia na serikali ya Syria na kwamba ubalozi wa nchi hiyo mjini Cairo utafungwa mara moja. Rais Mursi amekuwa miongoni mwa viongozi wa Kiarabu waliochukua misimamo ya kufurutu mipaka dhidi ya serikali ya Syria. Kwenye hotuba yake hapo jana mjini Cairo, Mursi alisema atamuita nyumbani balozi wa Misri kufuatia uamuzi huo. Weledi wa mambo wanasema hatua ya Misri itazidi kuvuruga hali ya mambo nchini Syria haswa kwa kuzingatia kwamba Misri ilikuwa katika kundi la nchi 4 zilizopewa jukumu la kufuatilia kadhia ya Syria kwa njia za kidiplomasia. Nchi zingine kwenye kundi hilo ni Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Uturuki na Saudi Arabia. Huku hayo yakijiri, habari zinasema jeshi la Syria limezidi kusonga mbele katika mji wa Allepo na kwamba linaendelea kupata mafanikio makubwa. Hii ni katika hali ambayo, Marekani inapanga kuanza kutuma silaha kwa magaidi wa Syria ili kukabiliana na jeshi la nchi hiyo. Wakati huo huo, serikali ya Russia imeionya Marekani dhidi ya kuweka marufuku ya kupaa ndege huko Syria ikisema jambo hilo litakuwa ukiukaji wa sheria za kimataifa.  

No comments:

Post a Comment