Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, July 5, 2013

Assad: Wapinzani wangu wameshindwa kunipindua


Assad: Wapinzani wangu wameshindwa kunipindua
Rais Bashar la Assad wa Syria amesema kuwa, wapinzani wake wameshindwa kumpindua ijapokuwa wametumia zana zote walizonazo. Assad amekataa kuitwa matukio yanayojiri nchini Syria kwa zaidi ya miaka miwili kuwa harakati za mapinduzi na badala yake amesisitiza kuwa, ni njama za Wamagharibi na baadhi ya nchi za Kiarabu za kuidhoofisha nchi yake. Aidha Rais wa Syria amepongeza maandamano makubwa ya Wamisri yaliyopelekea kungushwa serikali ya rais Muhammad Musri na kusema kwamba hatua hiyo ni mafanikio makubwa.
 Hayo yamejiri huku muungano wa wapinzani wa Syria (SNC) unaoungwa mkono na nchi za Magharibi kwa mara nyingine ukifanya jitihada za kuungana na kumchagua kiongozi mpya katika mkutano unaofanyika mjini Istanbul.

No comments:

Post a Comment