Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, July 19, 2013

OIC: Wakazi wa Gaza, Palestina wasaidiwe


Nitajiandaa vipi kwa ajili ya mitihani bila umeme?Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC imetoa wito wa kuungwa mkono wakazi wa Ukanda wa Gaza huko Palestina ambao wanakabiliwa na mzingiro. Taarifa ya OIC imewataka walimwengu kuwaunga mkono kwa kuwapatia misaada wananchi wa Gaza ambao kwa sasa wako katika hali mbaya ya kibinadamu. Wito huo wa OIC ambao umekuja baada ya ripoti yake kuhusiana na hali ya kibinadamu huko Gaza katika mwezi uliopita wa Juni, imesisitiza juu ya udharura wa kusaidiwa wananchi hao ili waweze kujidhaminia mahitaji muhimu kama ya chakula, maji, umeme na madawa. Ripoti ya Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC imebainisha kwamba, hali ya kibinadamu huko Gaza inazidi kuwa mbaya na kwamba, kama hali itaendelea hivyo, basi hadi kufikia mwaka 2020, eneo la Ukanda wa Gaza litakumbwa na maafa ya kibinadamu na wakazi wa eneo hilo hawataweza kupata maji ya kunywa hata tone moja kutokana na kuendelea kuharibika vibaya miundo mbinu ya maji na umeme.  Eneo la Ukanda wa Gaza huko Palestina lina takribani wakazi milioni mbili na linakabiliwa na uhaba mkubwa wa mafuta, kukatikatika umeme na uhaba wa maji katika kipindi hiki cha msimu wa joto kali. Utawala wa Kizayuni usio na huruma, ulianza kutekeleza mzingiro dhidi ya Gaza tangu mwaka 2007 na hali ya kibinadamu katika eneo hilo imezidi kuwa mbaya siku baada ya siku.

No comments:

Post a Comment