Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, July 19, 2013

Ramadhani yapandisha bei za vyakula Tanzania


Ramadhani yapandisha bei za vyakula Tanzania
Bei za vyakula katika mwezi huu wa Ramadhani zinaripotiwa kupanda nchini Tanzania hususan katika jiji la Dar es Salaam. Baadhi ya vyakula ambavyo hutumiwa na Waislamu kama futari zinaonekana kupanda mno katika masoko mbalimbali jijini Dar es Salaam. Taarifa zaidi zinasema, maeneo ya Dar es Salaam kama Tabata Kimanga, Bima na hata Segerea yanashuhudia bidhaa za vyakula zikiwa juu ukilinganisha na maeneo ya Kariakoo, Vingunguti na hata Magomeni. Bidhaa kama magimbi, viazi zinadaiwa kupanda kutokana na ugumu wa upatikanaji wake katika masoko. Baadhi ya wafanyabiashara wanasema, kwa kipindi hiki mahitaji ni makubwa kuliko upatikanaji wa bidhaa, na kwamba, hali hii imesababishwa na mvua kutokunyesha kwa wakati na kusababisha uhaba wa mavuno. Aidha katika mikoa mingine ya Tanzania pia kumeripotiwa kupanda bei za vyakula vya mwezi wa Ramadhani kama mihogo, magimbi, viazi na maboga. Baadhi ya wafanyabiashara pia wamekuwa wakilangua kwa makusudi vyakula wakifahamu kwamba, katika kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani bidhaa hizo zinahitajika sana.

No comments:

Post a Comment