Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, July 19, 2013

Uvamizi wa Wazayuni al-Aqswa walaaniwa


Uvamizi wa Wazayuni al-Aqswa walaaniwaSerikali halali iliyochaguliwa na wananchi ya Palestina imelaani uvamizi wa mara kwa mara wa Wazayuni dhidi ya Msikiti wa al-Aqswa. Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Masuala ya Quds katika Wizara ya Mambo ya Ndani na Usalama wa Taifa wa Serikali ya Palestina inayoongozwa na Waziri Mkuu Ismail Hania imebainisha kwamba, utawala wa Kizayuni wa Israel umeendelea kufanya uvamizi wa mara kwa mara katika mji wa Quds na dhidi ya msikiti mtakatifu wa al-Aqswa. Taarifa hiyo imebainisha kwamba, mipango na njama zote za adui Mzayuni zitashindwa kwani eneo hilo takatifu ni mali ya Waislamu wote ulimwengu. Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa, Waislamu kote ulimwenguni wanapaswa kuuhami msikiti wa al-Aqswa na kutouruhusu utawala  wa Kizayunio wa Israel kufikia malengo yake haramu.

No comments:

Post a Comment