Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, July 19, 2013

UN yataka utulivu urejeshwe Guinea Conakry

UN yataka utulivu urejeshwe Guinea ConakryKatibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito wa kurejeshwa amani na utulivu huko Guinea Conakry baada ya makumi ya watu kuuawa kufuatia mapigano ya kikabila yaliyotokea katika mji mmoja nchini humo. Ban ki-Moon kupitia msemaji wake ameeleza wasi wasi mkubwa ulionao Umoja wa Mataifa kuhusiana na mapigano ya kikabila yaliyozuka katika mji wa N'Zerekore ambao ni wa pili kwa idadi kubwa ya watu nchini humo baada ya mji mkuu Conakry. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewataka wananchi wa nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika kudumisha utulivu na amani na kujiepusha na hatua yoyote ile yenye kupelekea amani na usalama kuwa hatarini. Aidha Ban ki-Moon amewataka viongozi wa kitaifa na kikabila kulinda kudhamini usalama wa roho na mali za watu na kuheshimu sheria. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito pia wa kuandaliwa mazingira mazuri kwa ajili ya uchaguzi wa Bunge uliopangwa kufanyika mwezi Septemba mwaka huu. Zaidi ya watu  54 wameuawa hadi sasa  katika mapigano makali ya kikabila yaliyotokea katika mji wa N'Zerekore nchini Guinea Conakry. Inaelezwa, mapigano hayo yalianza baada ya watu wa kabila la Guerze kumpiga na kumuua kijana mmoja wa ukoo wa Konianke kwa tuhuma za wizi.

No comments:

Post a Comment