Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, July 26, 2013

Iran yaomboleza ajali ya treni ya Uhispania


Iran yaomboleza ajali ya treni ya Uhispania
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa mkono wa pole kwa serikali na wananchi wa Uhispania kutokana na ajali ya treni iliyotokea hivi karibuni nchini humo na kupelekea watu wasiopungua 80 kufariki dunia na wengine wasiopungua 140 kujeruhiwa 20, kati ya hali zao mahututi. Sayyid Abbas Araqchi Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa, ajali hiyo ya treni imeleta majonzi ulimwenguni kote, hivyo serikali pamoja na wananchi wa Iran wanaungana na wenzao wa Uhispania kwenye kipindi hiki kigumu cha huzuni na maombelezo. Ajali hiyo ilitokea siku ya Jumatano, pale treni hiyo kutembea mwendo wa kasi  katika kona na kusababisha mabehewa 13 kuondoka kwenye reli, na manne kupinduka kabisa. Taarifa zinasema kuwa, dereva wa treni hiyo anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi, ingawa alishatoa tahadhari ya kuanguka kwa treni hiyo, baada ya kushindwa kuidhibiti treni hiyo iliyokuwa kwenye  mwendo wa kasi kubwa. Treni hiyo ilikuwa ikitoka Madrid na kuelekea El Ferrol, na kupata ajali katika mji wa Santiago de Compestela, ulioko katika mkoa wa Galicia. Hii inahesabiwa kuwa ajali mbaya zaidi ya treni kutokea nchini humo tokea mwaka 1972.

No comments:

Post a Comment