Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, July 5, 2013

Wafuasi wa Mursi kuandamana leo Misri


Wafuasi wa Mursi kuandamana leo Misri
Maandamano ya mirengo ya Kiislamu yaliyoitishwa na harakati ya Ikhawanul Muslimin ya Misri yanatarajiwa kufanyika leo nchini humo baada ya mshuko wa swala ya Ijumaa, ili kupinga hatua ya jeshi ya kumuuzulu rais Muhammad Mursi.  Ikhawanul Muslimin ya Misri jana iliwataka wananchi wa nchi hiyo kuandamana kwa amani baada ya swala ya Ijumaa katika maandamano yaliyopewa jina la 'Ijumaa ya Kukataa'. Maandamano hayo yataonesha ni kwa kiwango gani rais huyo aliyeuzuliwa bado anaungwa mkono na wananchi, na pia hatua zitakazochukuliwa na jeshi kukabiliana nayo.
Muhammad Musri kiongozi aliyeondolewa madarakani wa Misri anatoka katika harakati ya Ikhwanul Muslimin na alikuwa rais wa kwanza kuchaguliwa kidemokraia  na Wamisri baada ya mapinduzi ya wananchi yaliyomng'oa madarakani dikteta Hosni Mubarak.

No comments:

Post a Comment