Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, July 5, 2013

Serikali ya Kongo DRC yaazimia kukabiliana na M23


Serikali ya Kongo DRC yaazimia kukabiliana na M23
Serikali ya Jamhuri ya Kidomekrasia ya Kongo imetangaza kuwa itakabiliana vilivyo na vitisho vya waasi wa M23 nchini humo. Lambart Mende msemaji wa serikali ya Kongo DRC jana alitangaza kuwa, serikali ya Kinshasa inavizingatia vitsho vya waasi wa M 23 hasa baada ya waasi hao kuuteka tena mji wa Goma, ambao ni makao makuu ya mkoa wa Kivu Kaskazini.
Msemaji huyo wa serikali ya Kongo ameongeza kwamba, suluhisho pekee kwa waasi hao ni kuendelea na mazungumzo ya kusaka amani huko Kampala Uganda na kuwatahadharisha kuwa, vikosi vya Umoja wa Mataifa viko katika eneo la Mashariki ya Kongo ambako vinashirikiana na wanajeshi wa Kongo, hivyo ni bora M23 waache machafuko.

No comments:

Post a Comment