Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, July 17, 2013

HUYU NDIYO IMAMU ALIYEMALIZA QUR-AN YOTE RAMADHANI YA PILI KATIKA SWALA YA TARAWEHE.


Imamu wa Msikiti Mkubwa uliyopo kusini nchini Saudi arabia, Sheikh Ahmad Hawashi, alifanikiwa kuhitimisha Qur-an yote juzu 30 ramadhani ya pili kwa tarawehe Tatu, kawaida swala ya tarawehe huanza usiku unaonekana mwezi.
Kwa mujibu wa Gazeti la Ambaa la nchini Kuwait, Sheikh Hawashi ni maarufu kwa kurefusha swala ya tarewehe, na kawaida uhitimisha Qur-an mara 10 kila Ramadhan.
Imamu huyo alirefusha swala hiyo ya tarawehe mpaka karibu na swala ya alfajiri.
Sheikh Hawashi kitaluma alihitimu masomo ya sayansi katika shule ya sekondari na aliwai kuajiliwa na Taasisi ya kuamrisha mema na kukataza maovu, kutoka na utenaji wake mzuri wa kazi, Sheikh Hawashi aliteuliwa kuwa Msaidizi wa rais wa taasisi hiyo.

No comments:

Post a Comment