Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, July 24, 2013

US yaitaka Rwanda isiwasaidie waasi wa M23


US yaitaka Rwanda isiwasaidie waasi wa M23
Marekani imeitaka Rwanda kuacha kuwaunga mkono waasi wa Machi 23 huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Washington imesema, kuna ushahidi kwamba maafisa wa jeshi la Rwanda wanawasaidia waasi wa M23. Hii ni radiamali ya kwanza kutolewa na Washington kufuatia mapigano yaliyojiri hivi karibuni kati ya waasi wa M23 na vikosi vya serikali ya Kinshasa karibu na mji wa Goma, ambao ndio mji mkubwa zaidi huko mashariki mwa Kongo na ni eneo tajiri kwa madini. Jen Psaki, msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani amesema, Washington inaitaka Rwanda iache mara moja kuwaunga mkono waasi wa Machi 23 na kuondoa vikosi vyake huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Wito huo umetolewa ikiwa zimesalia siku tatu kabla ya John Kerry, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani kuwa mwenyekiti wa kikao maalumu cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kitakachojadili eneo la maziwa makuu ya Afrika.  

No comments:

Post a Comment