Bandar bin Sultan bin AbdulAziz Mkuu wa Shirika la Kijasusi la 
Saudi Arabia ameelekea nchini Russia kwa shabaha ya kupanga mikakati 
mipya dhidi ya serikali ya Syria. Taarifa zinasema kuwa, safari ya 
Bandar bin Sultan ina lengo la kufanya njama za kukwamisha kikao cha 
Geneva 2 na kuimarisha nguvu za wapinzani na makundi ya kigaidi 
yanayopambana na serikali ya Syria. Itakumbukwa kuwa, Mwanamfalme huyo 
wa Saudi Arabia alionyesha radiamali kali baada ya kufikiwa makubaliano 
ya awali ya nyuklia kati ya Iran na kundi la 5 + 1 mjini Geneva hivi 
karibuni. Hii ni mara ya pili kwa Bandar bin Sultan kufanya safari 
nchini Russia katika kipindi cha miezi minne iliyopita. Katika safari 
iliyopita, alitoa pendekezo kwa viongozi wa Russia la kuitaka nchi hiyo 
iache kuiunga mkono Syria, mkabala wa Saudi Arabia kununua silaha na 
zana za kijeshi zenye thamani ya dola bilioni 15, pendekezo ambalo 
lilipingwa vikali na viongozi wa Moscow. Saudi Arabia inawapatia misaada
 ya kifedha na kisilaha makundi ya Geneva
Kisalafi na yale yanayowakufurisha Waislamu wengine, kwa lengo la kushadidisha machafuko nchini Syria, na hatimaye kuangushwa utawala wa Rais Bashar Assad wa nchi hiyo.
   
Kisalafi na yale yanayowakufurisha Waislamu wengine, kwa lengo la kushadidisha machafuko nchini Syria, na hatimaye kuangushwa utawala wa Rais Bashar Assad wa nchi hiyo.







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment