Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, December 7, 2013

Ufaransa yaunga mkono kuundwa 'kikosi kazi' Afrika


Ufaransa yaunga mkono kuundwa 'kikosi kazi' Afrika
Serikali ya Ufaransa imeeleza azma ya kushiriki nchi hiyo kwenye uundwaji wa kikosi cha kijeshi cha Kiafrika cha kutoa radiamali haraka ifikapo mwaka 2015. Hayo yameelezwa na Laurent Fabius Waziri wa Mamb ya Nchi za Nje na Jean Yves Le Drian Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa pambizoni mwa kikao cha siku mbili cha kujadili amani na usalama barani Afrika, kinachohudhuriwa na wakuu wa nchi za Kiafrika. Wakuu wengi wa Kiafrika waliohutubia kikao hicho hapo jana  wamesema kuwa, hivi sasa Waafrika hawana uwezo wa kulinda amani na usalama wa bara hilo. Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ufaransa amesema kuwa, wakuu wa nchi za Kiafrika kwa kauli moja wameafikiana  suala la kupambana na makundi ya kigaidi na maharamia katika Ghuba ya Guinea. Naye Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa amesema kuwa, kuna udharura wa kuundwa kikosi cha kutoa radiamali haraka barani Afrika kitakachokuwa chini ya usimamizi wa Umoja wa Afrika na kusisitiza kuwa, Paris inaunga mkono kikamilifu suala hilo. Jean Yves Le Drian amesema kuwa suala la maharamia katika Ghuba ya Guinea litajadiliwa kwenye Baraza la Ulaya hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment