Serikali ya Ufaransa imeeleza azma ya kushiriki nchi hiyo kwenye 
uundwaji wa kikosi cha kijeshi cha Kiafrika cha kutoa radiamali haraka 
ifikapo mwaka 2015. Hayo yameelezwa na Laurent Fabius Waziri wa Mamb ya 
Nchi za Nje na Jean Yves Le Drian Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa pambizoni
 mwa kikao cha siku mbili cha kujadili amani na usalama barani Afrika, 
kinachohudhuriwa na wakuu wa nchi za Kiafrika. Wakuu wengi wa Kiafrika 
waliohutubia kikao hicho hapo jana  wamesema kuwa, hivi sasa Waafrika 
hawana uwezo wa kulinda amani na usalama wa bara hilo. Waziri wa Mambo 
ya Nchi za Nje wa Ufaransa amesema kuwa, wakuu wa nchi za Kiafrika kwa 
kauli moja wameafikiana  suala la kupambana na makundi ya kigaidi na 
maharamia katika Ghuba ya Guinea. Naye Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa 
amesema kuwa, kuna udharura wa kuundwa kikosi cha kutoa radiamali haraka
 barani Afrika kitakachokuwa chini ya usimamizi wa Umoja wa Afrika na 
kusisitiza kuwa, Paris inaunga mkono kikamilifu suala hilo. Jean Yves Le
 Drian amesema kuwa suala la maharamia katika Ghuba ya Guinea 
litajadiliwa kwenye Baraza la Ulaya hivi karibuni.
   
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment