Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, December 12, 2013

Wahajiri wa Kiafrika wafungwa jela bila mashtaka Israel


Wahajiri wa Kiafrika wafungwa jela bila mashtaka Israel
Utawala wa Kizayuni wa Israel umewafunga jela wahajiri 480 wa Kiafrika, na idadi hiyo inaweza kuongezeka hadi kufikia 1,000 mwishoni mwa mwaka huu. Kwa mujibu wa sheria iliyopitishwa na Bunge la Israel wiki iliyopita, viongozi wa Israel wanaweza kuwaweka korokoroni wahajiri wa Kiafrika kwa muda wa mwaka mmoja bila ya kuwafungulia mashtaka. Hivi karibuni, utawala wa Kizayuni wa Israel ulipitisha mpango mpya ulio dhidi ya wahajiri elfu hamsini wa Kiafrika, ambao unatoa adhabu kali dhidi ya Waafrika wanaofanya kazi huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu. Wakati huohuo, Taasisi ya Wahajiri ya Israel imeeleza kuwa, tokea kuanza mwaka huu wa 2013 zaidi ya wahajiri 1,600 kutoka Eritrea na Sudan wamefukuzwa huko Israel na kurejeshwa makwao. Hayo yanajiri katika hali ambayo, wahajiri wa Kiafrika wameshafanya maandamano mara kadhaa wakilalamikia vitendo hivyo vya kibaguzi na unyanyasaji, ingawa waandamanaji hao wamekuwa wakishambuliwa kwa mabomu ya machozi na risasi za plastiki na vikosi vya usalama vya Israel.

No comments:

Post a Comment