Idadi kadhaa ya wapiganaji dhidi ya serikali ya Jamhuri
 ya Kidemokrasia ya Kongo, wamejisalimisha kwa vikosi vya Kimataifa 
nchini humo. Vikosi vya Kimataifa vya kulinda amani nchini Kongo 
vimetangza kuwa, wapiganaji hao wamejisalimisha kufuatia operesheni kali
 zilizoanzishwa na majeshi hayo ya UN huko katika maeneo ya mashariki 
mwa Kongo na mpakani na Rwanda. Baada ya vikosi vya Kimataifa kwa 
kushirikiana na vikosi vya serikali ya Kongo kuwashinda wapiganaji wa 
Harakati ya M23 hivi karibuni, vikosi hivyo vimeazimia kuwaondoa 
wapiganaji wa Kihutu kutoka katika maeneo ya mashariki na katika mipaka 
ya pamoja na nchi ya Rwanda. Hivi karibuni Martin Kobler, Mkuu wa 
Operesheni ya Umoja wa Mataifa ya Kurejesha Amani nchini Kongo MONUSCO 
amethibitisha kuanza kwa operesheni hizo kali dhidi ya waasi wa Rwanda 
nchini Kongo tarehe 27 Novemba mwaka huu. Tangu mwaka 1990 mamilioni ya 
watu huko mashariki mwa Kongo wamekwishapoteza maisha yao kutokana na 
mapigano au njaa. Maeneo ya mashariki mwa Kongo yanatajwa kuwa na 
utajiri mwingi wa dhahabu, urani, alimasi na madini ya shaba.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment