Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, December 12, 2013

Wanamgambo wajisalimisha kwa vikosi vya UN Kongo


Wanamgambo wajisalimisha kwa vikosi vya UN Kongo
Idadi kadhaa ya wapiganaji dhidi ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wamejisalimisha kwa vikosi vya Kimataifa nchini humo. Vikosi vya Kimataifa vya kulinda amani nchini Kongo vimetangza kuwa, wapiganaji hao wamejisalimisha kufuatia operesheni kali zilizoanzishwa na majeshi hayo ya UN huko katika maeneo ya mashariki mwa Kongo na mpakani na Rwanda. Baada ya vikosi vya Kimataifa kwa kushirikiana na vikosi vya serikali ya Kongo kuwashinda wapiganaji wa Harakati ya M23 hivi karibuni, vikosi hivyo vimeazimia kuwaondoa wapiganaji wa Kihutu kutoka katika maeneo ya mashariki na katika mipaka ya pamoja na nchi ya Rwanda. Hivi karibuni Martin Kobler, Mkuu wa Operesheni ya Umoja wa Mataifa ya Kurejesha Amani nchini Kongo MONUSCO amethibitisha kuanza kwa operesheni hizo kali dhidi ya waasi wa Rwanda nchini Kongo tarehe 27 Novemba mwaka huu. Tangu mwaka 1990 mamilioni ya watu huko mashariki mwa Kongo wamekwishapoteza maisha yao kutokana na mapigano au njaa. Maeneo ya mashariki mwa Kongo yanatajwa kuwa na utajiri mwingi wa dhahabu, urani, alimasi na madini ya shaba.

No comments:

Post a Comment