Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, December 30, 2013

Watu 15 wauawa katika mlipuko wa basi Russia


Watu 15 wauawa katika mlipuko wa basi Russia
Watu wasiopungua 15 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika mlipuko uliotokea ndani ya basi la abiria mapema leo katika mji wa Volgograd huko kusini mwa Russia.
Mlipuko huo umetokea wakati basi hilo lilipokuwa linakaribia soko la mji huo la umeharibu viyoo vya nyumba jirani.
Naibu Gavana wa mji wa Volgograd, Vasily Galushkin amesema ripoti alizonazo zinasema kuwa watu 15 wameuawa katika mlipuko huo na makumi ya wengine kujeruhiwa. Wataalamu wa serikali ya Russia wanasema kuwa mlipuko huo umetokana na shambulizi la kigaidi.
Shambulizi hilo limetokea siku moja tu baada ya hujuma nyingine ya bomu katika kituo kikuu cha treni cha mji wa Volgograd ambayo imesababisha vifo vya watu 17 na kujeruhi wengine wengi.
Hadi sasa hakuna mtu au kundi lililodai kuhusika na mashambulizi hayo ambayo yamefanyika kabla ya michezo ya Olimpiki ya msimu wa baridi ya Sochi iliyopangwa kufanyika mwezi Fubruari mwakani.

No comments:

Post a Comment