Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, December 7, 2013

'Libya huenda itakabiliwa na hatima ya Somalia'


'Libya huenda itakabiliwa na hatima ya Somalia'
Rais Mahamadou Issoufou wa Niger ametahadharisha uwezekano wa Libya kutumbukia kwenye machafuko makubwa zaidi kama ilivyowahi kuikumba  Somalia. Akizungumza pambizoni mwa kikao cha usalama na amani barani Afrika huko Paris  nchini Ufaransa, Rais Issoufou ameongeza kuwa, hali ya Libya ni tete mno kwani harakati za makundi ya kigaidi na wanamgambo wa Kisalafi zinazidi kuongezeka na kuuawa makumi ya watu kila uchao katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo. Rais wa Niger amesisitiza udharura wa kurejeshwa amani na utulivu nchini humo. Niger ambayo inapakana na Libya upande wa kusini, imekuwa ikikabiliana na makundi yenye kuchupa mipaka ndani ya ardhi ya Niger ikisaidiana na washirika wake wa Magharibi na nchi majirani.

No comments:

Post a Comment