Rais Mahamadou Issoufou wa Niger ametahadharisha uwezekano wa 
Libya kutumbukia kwenye machafuko makubwa zaidi kama ilivyowahi kuikumba
  Somalia. Akizungumza pambizoni mwa kikao cha usalama na amani barani 
Afrika huko Paris  nchini Ufaransa, Rais Issoufou ameongeza kuwa, hali 
ya Libya ni tete mno kwani harakati za makundi ya kigaidi na wanamgambo 
wa Kisalafi zinazidi kuongezeka na kuuawa makumi ya watu kila uchao 
katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo. Rais wa Niger amesisitiza 
udharura wa kurejeshwa amani na utulivu nchini humo. Niger ambayo 
inapakana na Libya upande wa kusini, imekuwa ikikabiliana na makundi 
yenye kuchupa mipaka ndani ya ardhi ya Niger ikisaidiana na washirika 
wake wa Magharibi na nchi majirani.
   
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment