Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, December 30, 2013

Maandamano yaendelea Misri, makumi wajeruhiwa


Maandamano yaendelea Misri, makumi wajeruhiwa
Wanafunzi wa vyuo vikuu vya Misri wameendelea kuandamana leo wakipinga ukandamizaji uliofanywa na vyombo vya usalama dhidi ya wanafunzi wenzao wa Chuo Kikuu cha al Azhar mjini Cairo katika siku chache zilizopita.
Maandamano haya yanafanyika huku idadi ya watu waliojeruhiwa katika machafuko ya jana mjini Cairo ikiendelea kuongezeka. Idadi kubwa ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha al Azhar walijeruhiwa baada ya askari usalama wa serikali ya mpito ya Misri kushambulia uwanja wa chuo hicho na kutawanya wanafunzi waliokuwa wakiandamana kupinga mapinduzi ya kijeshi yaliyoiondoa madarakani serikali ya Muhammad Mursi.
Jeshi la Misri limewakamata wanafunzi kadhaa wa Kitengo cha Biashara cha Chuo Kikuu cha al Azhar siku moja baada ya polisi kuua mwanafunzi mmoja na kujeruhi wengine kadhaa katika jaribio la kutawala maandamanao ya wanafunzi wanaopinga utawala unaoungwa mkono na jeshi la Misri.

No comments:

Post a Comment