Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, May 14, 2012

TUNA LAANI UDHAMINI WA KAMPUNI YA ULEVI

Pia, udhamini huu umeleta idhilali na fedheha kubwa itakayowagaeuza vijana wa umma mtukufu wa kiislamu kuwa vibarua kwa gharama duni (thamanu bakhiys) kuitangaza kampuni ya ulevi ili izidi kuendeleza maovu mengi katika jamii ya Kiislamu na wanaadamu kwa jumla. Yametendeka haya ilhali unajuulikana wazi uharamu wa ulevi Kiislamu, ikiwemo kuutengeza, kuuza, kuusafirisha, kuutangaza nk. Na zaidi ya yote Uislamu umeweka bayana kwamba ulevi ndio mama wa maovu yote, na ni kazi ya Shetani. Adui mkubwa anayeshika bendera ya kupotosha Waislamu na wanadamu kwa ujumla.
Kumb: 1433/02 15 Jumadul Than, 1433 06 /05/2012
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TUNALAANI UDHAMINI WA KAMPUNI YA ULEVI
Hizb ut-Tahrir Afrika Mashariki imeipokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya karibuni ya kupatiwa udhamini Kampuni ya Ulevi Tanzania (TBL) kuidhamini Ligi kuu ya mpira wa miguu Zanzibar. Udhamini utakaochukua muda wa miaka mitatu kwa thamani duni ya Shillingi Milioni 140.
Aidha, Hizb inalaani vikali udhamini huo uliofanywa kijanja kwa kisingizio cha kinywaji cha Grand Malt. Udhamini huu ni dalili ya kutojali kwa Serikali na wizara husika msimamo wa raia kupinga udhamini wa kampuni za ulevi. Jambo ambalo ni kinyume na Uislamu, imani ya walio wengi katika raia.
Pia, udhamini huu umeleta idhilali na fedheha kubwa itakayowagaeuza vijana wa umma mtukufu wa kiislamu kuwa vibarua kwa gharama duni (thamanu bakhiys) kuitangaza kampuni ya ulevi ili izidi kuendeleza maovu mengi katika jamii ya Kiislamu na wanaadamu kwa jumla. Yametendeka haya ilhali unajuulikana wazi uharamu wa ulevi Kiislamu, ikiwemo kuutengeza, kuuza, kuusafirisha, kuutangaza nk. Na zaidi ya yote Uislamu umeweka bayana kwamba ulevi ndio mama wa maovu yote, na ni kazi ya Shetani. Adui mkubwa anayeshika bendera ya kupotosha Waislamu na wanadamu kwa ujumla.
إِنَّمَا يُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَنْ يُوقِعَ بَيْنَكُمْ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ فِي الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ وَيَصُدَّكُمْ عَنْ ذِكْرِ اللَّهِ وَعَنْ الصَّلاَةِ فَهَلْ أَنْتُمْ مُنتَهُونَ
“Hakika shetani anataka kukutilieni uadui na bughdha baina yenu kwa ulevi na kamari, na anataka kukuzuilieni kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kukuzuilieni kuswali. Basi je mtaacha ?”
Masoud Msellem
Naibu Mwakilishi kwa Vyombo vya Habari
Hizb ut-Tahrir Afrika Mashariki

No comments:

Post a Comment