Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, May 8, 2012

zanziar hatugawiki tena

KUNA WANAODHANI WANAWEZA TENA
KUTUGAWA WAZANZIBAR KWA KUTUMIA
MBINU ZILIZOPITWA NA WAKATI ZA ETI
KUSEMA KIZAZI CHA SULTANI KINAJIPENYEZA
KUTAKA KURUDI KUITAWALA ZANZIBAR HUU NI
UJINGA NA KUTOKIKUJUWA WANACHOKISEMA
NA ZAIDI HAWAIJUI HII ZANZIBAR WAPI IPO NA
ILIPITA WAPI WAPI!

Walitakiwa wajuwe kwanza ni
sababu gani iliyomfanya mfalme
wa Oman kuja Afrika Mashariki
na kamuondoa Mreno.

Wareno walipoizuru pwani ya Afrika
Mashariki mwaka wa 1498
wakiongozwa na Vasco da Gama
katika juhudi yao ya kutafuta
njia ya Bahari ya kufika Bara
Hindi, walistaajabu sana kuona
kuwa takriban watu wote wa
Afrika Mashariki walikuwa ni
Waislamu.

Baada ya miaka michache
walipofaulu kuiweka Afrika
Mashariki chini ya himaya yao,
walianza harakati za kuuondoa
Uislamu kwa njia yoyote
waliyoweza kutumia.
Waislamu wa Afrika Mashariki, kuona
wanaendelea kunyanyaswa,
walikata shauri ya kutafuta
msaada wa kijeshi kutoka
nchi yoyote ya Kiislamu ili
wamwondoe Mreno.
Mikutano ya siri baina
ya Waislamu na makabila
mengine ya Afrika Mashariki
ikawa ikifanyika kutoka Lamu
Kaskazini mpaka Kilwa Kusini
ya upwa wote.
Mwisho wakakata shauri
kupeleka ujumbe wa siri kwa
mfalme wa Oman kutaka
msaada wake. Ujumbe wenyewe
ulikuwa ni wa watu wanane,
ukiongozwa na Mwinyi Nguti
wa Mwinyi Mwinzagu, Mzee
wa Waswahili wa Mombasa.
We n g i n e w a l i k u w a n i
Mwishahali bin Ndari, Maalim
Ndao bin Haji, Mwinyi Mole
bin Haji, Sheikh Ahmed AllMalindi na Mtomato wa Mtorogo
wote wa Mombasa, Kubo wa
Mwamzungu ambaye alikuwa
mzee wa Kidigo miongoni
mwa makabila ya Mijikenda ya
pwani ya Kenya na Shahame bin
Shoka aliyewawakilisha watu
wa kisiwa cha Pemba.

Ujumbe uliondoka Mombasa
mwaka wa 1660 na ukapokewa
kwa taadhima na Mfalme wa
Oman aliyekuwa akiitwa Imam
Sultan bin Seif Al-Yaarubi.
Mwaka wa 1661 Jeshi la
mabaharia na askari wa KiOman lilihujumu na kuteka mji
wa Mombasa lakini hawakuweza
kuwafukuza Wareno, Imam
Sultan alifariki.

O m a n i l i k a b i l i w a n a
mapigano ya wao wenyewe
kwa wenyewe. Baada ya miaka
kumi hivi mtawala mpya
akawa mwanawe Imam Sultan
aliyeitwa Seif bin Sultan AlYaarubi,
“Qaid-ul-Ardh”
Qaid ul Ardh akadhamiria kumaliza
kazi ilioanzishwa na marehemu
baba yake ya kuwaondoa
Wareno. Akabuni jeshi kubwa
la majahazi 18 yaliyobeba
askari 3,000 kutoka makabila
mbali mbali ya Mashariki ya
kati, Makabila ya Ki-Oman
kama vile Mazrui, Mundhry,
Jeneby, Shikely, Bassamy na
Maamry, askari wa kiajemi na
askari wa kibulushi. Amir Jeshi
aliyechaguliwa na Qaid-ul-Ardh
alikuwa ni jemedari maarufu
wa Ki-Baluchi kutoka pwani
ya Makaran katika jimbo la
Baluchistan la Uajemi.

Jemedari huyo alikuwa
akiitwa Jemedar Amir Shahdad
Chotah. Chotah akauteka mji
wa Mombasa lakini kwa vile
Wareno wote wa Mombasa
wapatao 2,500 walijifungia
ndani ya Ngome ya Mombasa,
hakuweza kuiteka ile ngome.
Chotah aliizunguka Ngome
hiyo kwa muda mrefu, Jeshi
la Jemedari Chotah lilifanikiwa
kuiteka Ngome hiyo baada ya
miezi 33. Jemedari Chotah
akawapata Wareno wanane tu
na Waswahili wachache.
Wengi wa Wareno waliuwawa
na kukimbia kuelekea Msumbiji,
hawakuweza kurudi tena. Wengi
wa makabila ya watu wa Oman
waliuwawa katika mapigano
ya kuwakomboa ndugu zao wa
Kiislamu chini ya utawala wa
Wareno. Kuanzia hapo ndio
watu wanyewe kwa ridhaa zao
wakataka ulinzi wa watu wa
Oman na hapo ndipo palipozidi
kuoana baina ya Waswahili na
watu wa Oman. Sio rahisi hivi
sasa kuweza kuwatenganisha
Wazanzibari na wa Oman kwa
vile ni watu wamoja ki-damu
na ki-dini.

No comments:

Post a Comment