Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, July 30, 2012

NYUDHURU ZA KUFUNGA



Nyudhuru za kuacha kufunga zinatofautiana na kila udhuru una hukumu yake, na hapa nitazielezea  nyudhuru hizo kwa ufupi.

1-    Hedhi (damu ya mwezi) na nifasi (damu ya uzazi), huu ni udhuru ambao unamlazimisha mwanamke kuacha kufunga, na inakuwa haramu kwake funga na iwapo atafunga haitosihi
2-      
(haitokubaliwa) funga yake, na ni wajibu kwake kulipa funga hiyo.

2- Maradhi au Safari. Na mwenye udhuru wa maradhi (yanayotibika kwa kawaida) pamoja na msafiri wanaruhusiwa kutokufunga na itawawajibikia kulipa. Amesema Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) :{{Atakaye kuwa katika mji katika huu mwezi (wa Ramadhani) afunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi (atimize) hisabu (ya siku alizoacha kufunga) katika siku nyingine. Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyo mazito.. .}} (2:185).      Na kama maradhi yatazidi au kumletea madhara iwapo atafunga basi itakuwa lazima kwake kutokufunga.

*Ama safari ambayo inaruhusiwa kwa sababu yake kutokufunga wanachuoni wengi wemesema: Ni safari ya siku mbili kwa ngamia au kwa mwendo wa miguu (mar-hala mbili) ambayo ni sawa na umbali wa takiribani kilomita (85km). Na ruhusa hii inapatikana kwa msafiri anayesafiri kwa chombo cha aina yoyote atakachosafiria,ijapo kwa dhahiri safari hiyo haimpi uzito wowote.


3- Vizee (vikongwe) na wenye maradhi sugu (yasiotarajiwa kupoa). Na haya mawili iwapo yana msababishia madhara basi ni katika udhuru na ruhusa ya kuacha kufunga, na itamlazimikia atoe fidia kwa kumlisha masikini kibaba (mudi) cha chakula (ambacho ni sawa na na uzito wa gramu 600g takiribani)au chakula kinacho mshibisha masikini mmoja kwa kila siku aliyoacha kufunga.

4- Waja wazito na wanyonyeshaji.
Nao ni katika wenye ruhusa ya kutokufunga, na inawabidi kulipa siku walizoshindwa kufunga kwa sababu ya udhuru huo.

5:Iliemzidia njaa au kiu na akahofia kuangamia, huu pia ni katika udhuru wa kuacha kufunga, bali wamesema wanachuoni kwamba: yule mwenye kuhofia kuangamia inakuwa kwake ni wajibu kufungua, na itamuwajibikia kulipa kama mgonjwa

No comments:

Post a Comment