Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, April 3, 2013

Shambulio la Taliban laua wa 44 Afghanistan


Wanamgambo wa Taliban nchini Afghanistan
Wanamgambo waasi waliokuwa wamevalia sare za jeshi la taifa la Afghanistan wameua watu 44 na kuwajeruhi wengine 100 baada ya kufanya shambulio dhidi ya majengo ya serikali katika jimbo la Farah. Gavana wa Jimbo la Farah Mohammad Akram Ekhpelwak amesema kuwa, kwa uchache washambuliaji wanane waliuawa kwenye shambulio hilo. Amesema kuwa, shambulio hilo lililofanywa na kundi la wanamgambo wa Taleban lilikuwa na lengo la kuwakomboa wapiganaji wenzao waliokuwa wamefikishwa mahakamani. Amesema kuwa, raia 34, wanajeshi sita na askari wanne wameuawa kwenye shambulio hilo. Ekhpelwak ameongeza kuwa, shambulio hilo lililenga majengo ya serikali zikiwemo ofisi ya mahakama na ile ya Mwanasheria Mkuu. 

No comments:

Post a Comment