Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, April 9, 2013

Chama cha Walimu Tanzania chaionya serikali


Chama cha Walimu Tanzania chaionya serikali Chama cha Walimu Tanzania (CWT), kimetaka Bunge na wazazi kuingilia kati uamuzi wa Serikali wa kukataa kukaa katika meza moja kwa ajili ya kuzungumzia nyongeza za mishahara na posho. Taarifa ya chama hicho imetahadharisha kuwa, vinginevyo Serikali inakaribisha mgomo mwingine wa walimu. Mwaka jana walimu nchini Tanzania waligoma kufanya kazi wakishinikiza nyongeza za mishahara, lakini Serikali ilikimbilia mahakamani. Aidha Mahakama ilisitisha mgomo huo kwa maelezo kuwa ulikuwa batili na baadaye, kuziagiza Serikali na CWT kukaa tena kwenye meza ya majadiliano. Rais wa Chama cha Walimu nchini Tanzania, Gratian Mukoba, amesema kuwa, pamoja na chama hicho kuwa tayari kuzungumza, Serikali ya Rais Kikwete imekataa kuzungumza nacho kuhusu nyongeza za mishahara na maslahi mengine ya walimu.

No comments:

Post a Comment