 Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limetangaza kuwa, 
wakimbizi sabini na nne elfu wa Mali wanahitajia msaada wa haraka wa 
kibinaadamu. Taarifa ya shirika hilo imeeleza kuwa, wakimbizi wa Mali 
walioko nchini Mali wanakabiliwa na hali mbaya zaidi ya kibinaadamu na 
kwamba, wanahitajia misaada ya haraka ili waweze kukidhi mahitaji yao 
muhimu. Ripoti ya shirika hilo sambamba na kutoa wito wa kupelekewa 
misaada kwa wakimbizi hao wa Mali imeeleza kwamba, wakimbiz hao 
wanakabiliwa na uhaba pamoja na ukata wa huduma muhimu kama maji na 
chakula. Matatizo makubwa ya wakimbizi hao ni uhaba wa maeneo ya 
kujihifadhi, upungufu wa chakula, maji safi ya kunywa,
Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limetangaza kuwa, 
wakimbizi sabini na nne elfu wa Mali wanahitajia msaada wa haraka wa 
kibinaadamu. Taarifa ya shirika hilo imeeleza kuwa, wakimbizi wa Mali 
walioko nchini Mali wanakabiliwa na hali mbaya zaidi ya kibinaadamu na 
kwamba, wanahitajia misaada ya haraka ili waweze kukidhi mahitaji yao 
muhimu. Ripoti ya shirika hilo sambamba na kutoa wito wa kupelekewa 
misaada kwa wakimbizi hao wa Mali imeeleza kwamba, wakimbiz hao 
wanakabiliwa na uhaba pamoja na ukata wa huduma muhimu kama maji na 
chakula. Matatizo makubwa ya wakimbizi hao ni uhaba wa maeneo ya 
kujihifadhi, upungufu wa chakula, maji safi ya kunywa, madawa na matibabu, imebainisha taarifa ya shirika hilo la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF). Hivi karibuni Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) ulitangaza kuwa, watoto wanaokaribia laki mbili wanakabiliwa na hatari ya kufariki dunia au kujeruhiwa na milipuko ya mabomu nchini Mali. UNICEF ilisema kuwa mabomu hayo ambayo bado hayajalipuka yamesalia nchini Mali tangu mwanzoni mwa mapigano yanayoendelea sasa kati ya vikosi vya majeshi ya Ufaransa na makundi yenye silaha katike eneo la kaskazini mwa Mali.







 
 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment