Mfungwa mwingine wa 
Kipalestina amekufa shahidi katika hali ya kutatanisha akiwa ndani ya 
gereza la kuogofya la Nafha huko Israel, Palestina inayokaliwa kwa 
mabavu.
Kufuatia kifo hicho, 
Wapalestina wanaoshikiliwa mateka katika magereza ya Utawala wa Kizayuni
 wa Israel waliitisha mgomo kwa lengo la kuwajuilisha walimwengu kuhusu 
hali yao mbaya inayowakabili. Mapema mwezi huu, Maisara Abu Hamdia,
 
mfungwa mwingine wa Kipalestina alikufa shahidi akiwa ndani ya gereza 
huko Israel. Mateka wapatao elfu 5 wa Kipalestina wanashikiliwa katika 
jela za utawala haramu na ghasibu wa Israel. Utawala huo ghasibu 
unaendelea kutekeleza siasa zake za kimabavu dhidi ya Wapalestina kwa 
kuwaua na kuwakandamiza raia wasiokuwa na hatia yoyote. Tangu mwaka 1948
 hadi hii leo, zaidi ya Wapalestina laki nane na nusu wamekamatwa na 
kuswekwa katika jela za kutisha za utawala wa Kizayuni. Kuendelea hatua 
za ukandamizaji za utawala wa Kizayuni dhidi ya mateka wa Kipalestina na
 udhaifu wa jumuiya za kimataifa katika kufuatilia faili la mateka hao 
kumezidisha machungu ya wananchi wanaokandamizwa wa Palestina. Hii ni 
katika hali ambayo jamii ya kimataifa imeendelea kunyamazia jinai za 
utawala haramu wa Israel, sambamba na utawala huo ghasibu kuungwa mkono 
na kusaidiwa na nchi za Magharibi.






 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment