Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, April 15, 2013

OIC yataka kutuma kamati yake nchini Myanmar


OIC yataka kutuma kamati yake nchini MyanmarJumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC imetoa wito wa kutumwa kamati ya jumuiya hiyo nchini Myanmar kwa shabaha ya kushuhudia kwa karibu hali inayowakabili Waislamu wa jamii ya Rohingya wa nchi hiyo. Taarifa ya mwisho ya mkutano wa kamati ya mawasiliano ya OIC imeitaka serikali ya Myanmar kuruhusu kamati ya mawaziri ya jumuiya hiyo kutumwa katika nchi hiyo. Akizungumza katika mkutano huo, Profesa Ekmeleddin İhsanoğluKatibu Mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC amesema kuwa, utumiaji mabavu unaofanywa dhidi ya Waislamu wa Myanmar haukubaliki hata kidogo na kwamba, hiyo ni ishara ya utendaji mbaya wa serikali ya nchi hiyo. Ni mwaka mmoja sasa ambapo OIC imekuwa ikitaka kutuma kamati ya uchunguzi nchini Myanmar lakini bado haijafanikiwa hadi sasa. Katika taarifa yake, Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC imeitaka Kamisheni ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa kutuma timu ya uchunguzi nchini Myanmar. Aidha OIC imezitaka nchi jirani na Myanmar kama Bangladesh na Malaysia kusaidia kutatua tatizo la Waislamu wa Rohingya wanaoandamwa na wimbi la mauaji yanayofanywa na Mabudha wenye misimamo mikali wakishirikiana na askari wa jeshi la serikali ya Myanmar.

Na Salum Bendera

No comments:

Post a Comment