Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, April 3, 2013

Utata wa uchinjaji waibua machafuko Tanzania


Maafisa wa polisi wakiondoa vizuzi vilivyowekwa na waandamanaji, Tunduma, Tanzania 03 Aprili 2013 
Vurugu na ghasia zimeripotiwa kutokea nchini Tanzania katika mji wa Tunduma mkoani Mbeya, baada ya vijana kuandamana mitaani na kuchoma moto matairi ya magari  na kuweka vizuizi mabarabarani wakipinga hatua ya viongozi wa dini ya Kikristo katika eneo hilo la mpakani kumuandikia barua Mkuu wa Wilaya ya Momba wakitaka wapewe ruhusa ya kuchinja wakati wa sherehe za Pasaka.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa, vijana wanaofanya kazi katika stendi ndio walioanzisha vurugu hizo majira ya asubuhi na kuvamiwa na jeshi la polisi lililotumia mabomu ya kutoa machozi ili kuwatawanya waandamanaji.

Hivi karibuni kulitokea machafuko na hata baadhi ya watu kuuawa na kujeruhiwa nchini Tanzania, baada ya Wakristo kutaka wachinje wanyama badalada ya Waislamu, jambo ambalo linapingwa na serikali na Waislamu.  Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda alinukuliwa akisema kuwa, utamaduni uliozoeleka nchini humo ni kwa Waislamu kuchinja nyama zinazouzwa mabuchani.

No comments:

Post a Comment