Vurugu na ghasia zimeripotiwa kutokea nchini Tanzania 
katika mji wa Tunduma mkoani Mbeya, baada ya vijana kuandamana mitaani 
na kuchoma moto matairi ya magari  na kuweka vizuizi mabarabarani 
wakipinga hatua ya viongozi wa dini ya Kikristo katika eneo hilo la 
mpakani kumuandikia barua Mkuu wa Wilaya ya Momba wakitaka wapewe ruhusa
 ya kuchinja wakati wa sherehe za Pasaka.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa, vijana wanaofanya kazi katika 
stendi ndio walioanzisha vurugu hizo majira ya asubuhi na kuvamiwa na 
jeshi la polisi lililotumia mabomu ya kutoa machozi ili kuwatawanya 
waandamanaji.
Hivi karibuni kulitokea machafuko na hata baadhi ya watu 
kuuawa na kujeruhiwa nchini Tanzania, baada ya Wakristo kutaka wachinje 
wanyama badalada ya Waislamu, jambo ambalo linapingwa na serikali na 
Waislamu.  Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda alinukuliwa akisema 
kuwa, utamaduni uliozoeleka nchini humo ni kwa Waislamu kuchinja nyama 
zinazouzwa mabuchani.







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment