Waziri wa Waqfu na Masuala ya Kidini wa serikali halali
 iliyochaguliwa na wananchi ya Palestina ametahadharisha kuhusiana na 
njama za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Masjidul Aqswa. Ismail 
Ridhwan amesisitiza kwamba, msikiti mtakatifu wa al-Aqswa uko katika 
hatua hatari mno kutokana na hujuma na mipango ya kujitanua ya Israel 
sambamba na hatua zake za kuuyahudisha mji wa Baytul Muqaddas. Waziri wa
 Waqfu na Masuala ya Dini wa serikali ya Palestina inayoongozwa na 
Waziri Mkuu Ismail Hania amewataka Waislamu kote ulimwengu kukabiliana 
na njama hizo za utawala ghasibu wa Israe. Ismail Ridhwan amezitaka nchi
 za Kiislamu na Kiarabu, Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Jumuiya ya 
Ushirikiano wa Kiislamu OIC,
 asasi za Kiislamu na maulama kwa ujumla 
kutekeleza majukumu yao ipasavyo na hivyo kusimama na kutetea matukufu 
ya Kiislamu. Ikumbukwe kuwa, mji wa Quds na msikiti mtakatifu wa 
al-Aqswa vimekuwa vikikabiliwa na njama za kila leo tangu utawala bandia
 wa Israel uasisiwe katika ardhi za Palestina miongo sita iliyopita.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment