Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, April 12, 2013

Njama za Wazayuni dhidi ya al-Aqswa zaendelea


Njama za Wazayuni dhidi ya al-Aqswa zaendelea
Waziri wa Waqfu na Masuala ya Kidini wa serikali halali iliyochaguliwa na wananchi ya Palestina ametahadharisha kuhusiana na njama za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Masjidul Aqswa. Ismail Ridhwan amesisitiza kwamba, msikiti mtakatifu wa al-Aqswa uko katika hatua hatari mno kutokana na hujuma na mipango ya kujitanua ya Israel sambamba na hatua zake za kuuyahudisha mji wa Baytul Muqaddas. Waziri wa Waqfu na Masuala ya Dini wa serikali ya Palestina inayoongozwa na Waziri Mkuu Ismail Hania amewataka Waislamu kote ulimwengu kukabiliana na njama hizo za utawala ghasibu wa Israe. Ismail Ridhwan amezitaka nchi za Kiislamu na Kiarabu, Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC,
asasi za Kiislamu na maulama kwa ujumla kutekeleza majukumu yao ipasavyo na hivyo kusimama na kutetea matukufu ya Kiislamu. Ikumbukwe kuwa, mji wa Quds na msikiti mtakatifu wa al-Aqswa vimekuwa vikikabiliwa na njama za kila leo tangu utawala bandia wa Israel uasisiwe katika ardhi za Palestina miongo sita iliyopita.

No comments:

Post a Comment