Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, April 15, 2013

Watu 20 wauawa katika machafuko C.A.R.


Watu 20 wauawa katika machafuko C.A.R.Watu wasiopungua 20 wameuawa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati na makumi ya wengine kujeruhiwa baada ya kuzuka machafuko katika mji mkuu wa nchi hiyo Bangui. Duru za hospitali, polisi na mashuhuda wanasema kuwa, watu hao wameuawa katika mapigano na machafuko tofauti yaliyotokea katika mji wa Bangui. Taarifa zaidi zinasema kuwa, watu 12 wameuawa katika Wilaya 7 za mji mkuu Bangui huku Shirika la Msalaba Mwekundu likiongeza kuwa, watu wengine wanne wameuawa katika maeneo mengine ya mji huo. Polisi imesema kuwa, mapigano hayo yalizuka wakati wanachama wa muungano wa waasi wa Seleka walipokuwa wakisaka silaha baina ya raia. Hayo yanajiri katika hali ambayo, Baraza la Mpito katika Jamhuri ya Afrika ya Kati limemuidhinisha kiongozi wa kundi la SELEKA, Michel Djotodia kuwa rais wa mpito wa nchi hiyo. Baraza hilo lenye wanachama 105 limemuidhinisha baada ya kukosekana mpinzani. Mwezi uliopita, Djotodia aliwaongoza waasi wa SELEKA kuipindua serikali ya Rais Francois Bozize ambaye kwa sasa anaishi uhamishoni nchini Benin.

Na Salum Bendera

No comments:

Post a Comment