Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, August 23, 2013

Kenya: Al Qaida inatayarisha shambulizi Mombasa


Kenya: Al Qaida inatayarisha shambulizi MombasaPolisi ya Kenya imetahadharisha kuwa kundi la kigaidi la al Qaida linajitayarisha kufanya mashambulizi katika mji wa pwani wa Mombasa katika kumbukumbu ya mauaji ya msomi wa Kiislamu Sheikh Aboud Rogo.
Taarifa ya polisi ya Kenya ambayo hadi sasa haijamtia nguvuni mtu aliyemuua msomi huyo wa Kiisalmu, imesema kuwa kundi la al Shabab linaloshirikiana na mtandano wa al Qaida, huenda linapanga kufanya mashambulizi ya kukumbuka kuuliwa msomi huyo.
Mkuu wa polisi ya kaunti ya Mombasa Robert Kitur amesema jeshi la polisi limepata taarifa za kipelelezi kuhusu tishio la shambulizi la kundi la al Shabab katika mji wa Mombasa katika kumbukumbu ya mauaji ya Sheikh Aboud Rogo. Kitur amesema usalama umeimarishwa zaidi katika mji wa Mombasa na kwamba polisi imezuiya maandamano ya kukumbuka tukio la kuuawa Sheikh Rogo.
Waislamu wengi wa Kenya wanaituhumi serikali ya nchi hiyo kwamba ilihusika na mauaji ya Sheikh Aboud Rogo yaliyofanyika Agousti 27 mwaka jana. Vyombo vya usalama vya Kenya hadi sasa havijamkamata mtu au watu waliofanya mauaji hayo.

No comments:

Post a Comment