Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, August 19, 2013

Waziri wa serikali ya Misri ateteta mauaji ya raia


Waziri wa serikali ya Misri ateteta mauaji ya raia
Nabil Fahmy, Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali ya mpito ya Misri iliyowekwa madarakani na jeshi ametetea ukandamizaji na umwagaji mkubwa wa damu uliofanywa hivi karibuni na jeshi dhidi  ya wafuasi wa Muhammad Morsi, rais wa nchi hiyo aliyeng’olewa madarakani na jeshi. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Cairo Fahmy amesema serikali ya mpito imeonyesha uvumilivu katika kukabiliana na waandamanaji na itaendelea kufanya hivyo. Matamshi hayo yametolewa huku Muungano Dhidi ya Mapinduzi unaojumuisha makundi kadhaa ikiwemo harakati ya Ikhwanul Muslimin ukijipanga kufanya maandamano mapya mjini Cairo. Zaidi ya watu 800 wameuawa na maelfu kadhaa kujeruhiwa katika ukandamizaji uliofanywa na jeshi na polisi ya Misri dhidi ya maandamano yaliyofanyika siku ya Jumatano na Ijumaa katika miji kadhaa ya Misri. Wakati huohuo jumuiya kadhaa za kutetea haki za binadamu ndani na nje ya Misri zinajiandaa kuchukua hatua ya kuwasilisha mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC dhidi ya Jenerali Abdulfatah al Sisi pamoja na maafisa wengine wa kijeshi na wa kiraia wa serikali ya mpito kwa kuhusika na mauaji ya hivi karibuni ya raia. Jumuiya hizo zimeeleza kuwa zinakusanya nyaraka na ushahidi ili kumfikisha katika Mahakama ya ICC Waziri wa Ulinzi al Sisi, Waziri wa Mambo ya Ndani Muhammad Ibrahim na maafisa wengine kadhaa wa jeshi…/

No comments:

Post a Comment