Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, August 8, 2013

Uwanja wa ndege Nairobi wafunguliwa baada ya moto


Uwanja wa ndege Nairobi wafunguliwa baada ya motoSafari za kimataifa za ndege zimeanza tena leo asubuhi katika Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi, Kenya baada ya eneo kubwa la uwanja huo kuteketezwa na moto siku ya Jumatano alfajiri.
Uwanja huo ulifungwa kwa muda jana na ndege zililazimika kutua Mombasa na katika nchi jirani.
Mkuu wa usalama katika uwanja wa Jomo Kenyatta Bw. Eric Kiraithe amesema wasafiri wa kimataifa watatumia eneo la wasafiri wa ndani ya nchi baada ya eneo la wasafiri wa kimataifa kuteketezwa kabisa katika moto wa jana. Taarifa zinasema zaidi ya wasafiri 16,000 ambao hupita katika uwanja huo kila siku waliathiriwa vibaya na mkasa huo wa moto.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya jana alifika katika uwanja huo wa ndege na kutoa taarifa kupitia msemaji wake Manoah Esipisu na kusema sababu za moto huo zinachunguzwa hivyo watu wajiepushe na uvumi. Alisema hatua zinachukuliwa kuhakikisha shughuli za uwanja huo zinarejea katika hali ya kawaida.

No comments:

Post a Comment