Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, August 13, 2013

Umasikini wa juu Saudi Arabia


Umasikini wa juu Saudi Arabia  Kiwango cha umasikini nchini Saudi Arabia kiko juu zaidi ya nchi za Lebanon, Jordan na Palestina. Hayo yamethibitishwa na mtaalamu mmoja wa masuala ya kiuchumi alipokuwa akizungumzia hali mbaya ya uchumi nchini Saudia na kusisitiza kuwa, kiwango cha umasikini katika nchi hiyo ya Kiarabu ni cha hali ya juu ukilinganisha na nchi za Lebanon, Jordan, Palestina, Tunisia na Syria. Aidha mtaalamu huyo wa masuala ya kiuchumi amesema kuwa, kiwango cha ukosefu wa ajira nchini humo nacho kiko juu zaidi ya nchi za Afrika. Mtaalamu huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kiwango hicho cha umasikini kilichopo nchini humo kinazidi hata zile nchi zinazopata misaada kutoka kwa Saudia yenyewe na kusisitiza kuwa, ripoti hiyo ipo pia hata katika mtandao wa benki ya dunia. Ameenda mbali zaidi na kusema kuwa, asilimia 99 ya wafanyakazi wengi wa serikali nchini humo wakiwemo maafisa wa jeshi na vyombo vya usalama, wanadaiwa na mabenki ya Saudia. Hii ni katika hali ambayo, Saudia ni mzalishaji mkubwa wa mafuta huku asilimia 70 ya utajiri wote wa nchi hiyo, ukielekea kwenye mifuko ya familia ya kifalme.

No comments:

Post a Comment