Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, August 8, 2013

Waingereza wawili wamwagiwa tindikali Zanzibar


Waingereza wawili wamwagiwa tindikali ZanzibarWanawake wawili raia wa Uingereza wamemwagiwa tindikali usoni Jumatano usiku mjini Zanzibar, Tanzania.
Imearifiwa kuwa wanawake hao wenye umri wa miaka 18 walishambuliwa na watu wasiojulikana walipokuwa wakitembea katika mitaa ya Stone Town. Duru zinaarifu kuwa washambuliaji walikuwa wanaume wawili waliopanda vespa.
Naibu Mkuu wa Polisi Zanzibar Mkadam Khamis amenukuliwa na AFP akisema, polisi wanawasaka waliotekeleza hujuma hiyo. Amesema sababu ya kushambuliwa raia hao wawili wa Uingereza haijabainika.
Katika siku za hivi karibuni kumeongezeka vitendo vya kuwamwagia watu tindikali nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment