Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, August 13, 2013

Waathiriwa wa mafuriko Sudan wapata misaada


Waathiriwa wa mafuriko Sudan wapata misaadaUmoja wa Mataifa umeanza kupeleka misaada ya kibinadamu kwa raia walioathiriwa mafuriko nchini Sudan. Mashirika ya misaada ya kibinadamu inayofungamana na Umoja wa Mataifa yameanza zoezi la upelekaji misaada hiyo kwa raia takribani laki moja na nusu waliokumbwa na mafuriko katika viunga vya mji mkuu Khartoum. Kifurushi cha awali cha misaada hiyo ya kibinadamu kinajumuisha chakula na maji safi ya kunywa. Raia hao wameathiriwa na mafuriko hayo kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini Sudan tangu mwanzoni mwa mwezi huu wa Agosti. Ripoti za utabiri wa hali ya hewa zinaonesha kuwa, mafuriko na mvua kali zitaendelea kunyesha katika siku kadhaa zijazo nchini Sudan na kuathiri idadi kubwa zaidi ya watu. Njia na barabara nyingi za mji wa Khartoum hazipitiki kutokana na kusambaa maji kila mahala huku sehemu kubwa ya mji mkuu huo ikiwa haina huduma ya maji na umeme kutokana na kuharibika miundo mbinu ya huduma hizo

No comments:

Post a Comment